BAADA YA UCHAGUZI WA MADIWANI KUTAWALIWA NA VURUGU,,MTOTO WA KIKWETE AIBUKA NA KUHOFIA AMANI YA NCHI ,SOMA HAPO KUJUA - Siasa News

Breaking

Siasa ni Maisha

Monday, 27 November 2017

BAADA YA UCHAGUZI WA MADIWANI KUTAWALIWA NA VURUGU,,MTOTO WA KIKWETE AIBUKA NA KUHOFIA AMANI YA NCHI ,SOMA HAPO KUJUA



WAKATI Uchaguzi mdogo wa Madiwani uliofanyika jana
nchi nzima kutajwa kugubikwa kwa vitendo vya utekaji
 kwa wabunge
wa Upinzani,pamoja na kufukuzwa kwa mawakala
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
 kwenye vituo vya kupiga kura, Hali hiyo imemubia
Mbunge wa jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CMM Mh. 
Ridhiwani Kikwete  baada ya kueleza kutofurahishwa na 
vitendo vya uvunjivu wa amani na migawanyiko,
vilivyojitokeza katika uchaguzi huo mdogo ambao
Chadema walisusika kata tano



“Siasa ya uchaguzi haipaswi kuwa mwanzo wa migawanyiko, mbegu tunayopanda leo kama haikukemewa itakuja kutusumbua siku sijazo, niwaombe Watanzania wenzangu, tudumishe upendo na tukatae fujo zisizo na lazima”, amesema Ridhiwani.
Aidha Ridhiwani ametoa ushauri unaolenga kuondoa visingizio na propaganda za kutumia wanachama kama ndio sehemu ya vurugu hizo akidai kuwa wafanya vurugu hao ni wananchi na sio CCM wala CHADEMA kama ambavyo kila upande unadai.

 “Wanaopigana ni wananchi, sio CCM wala CHADEMA, maana naona pande zote zinalalamika, tuwe na hukumu sahihi, la msingi tukatae fujo, nchi hii ni muhimu na tuenzi mawazo sahihi ya wazee wetu”, ameongeza Ridhiwani.
Wananchi katika Kata 43 za mikoa 19 nchini kote jana wamepiga kura kuchagua madiwani katika uchaguzi mdogo ambapo vitendo kadhaa vya vurugu viliripotiwa kutokea huku CHADEMA ikijitoa kushiriki uchaguzi huo katika kata 5 za wilaya ya Arumeru

No comments:

Post a Comment

Note: only a member of this blog may post a comment.