MKE WA MUGABE, GRACE MUGABE AMUOMBA MUME WAKE KUPOKEA NAFASI YA KUTAWALA ZIMBABWE - Siasa News

Breaking

Siasa ni Maisha

Monday, 6 November 2017

MKE WA MUGABE, GRACE MUGABE AMUOMBA MUME WAKE KUPOKEA NAFASI YA KUTAWALA ZIMBABWE


Grace Mugabe (File: AFP)

MKE WA MUGABE, GRACE MUGABE AMUOMBA MUME WAKE KUPOKEA NAFASI YA KUTAWALA ZIMBABWE

Mke wa Robert Mugabe(Grace Mugabe) amesema yupo tayari kupokea kijiti cha Urais kutoka kwa Mume  wake na amemuomba mume wake kumruhusu kuchukua nafsi hiyo. Zimbabwe wanatarajia kufanya uchaguzi mkuu mwaka 2018 ,watu wengi nchini Zimbabwe wamekuwa wakijiuliza nani atapokea kijiti cha Uraisi kutoka kwa Kiongozi Wa sasa Robert Mugabe ambaye Umri umeenda na hana vigezo vya kugombea tena, Hivi karibuni Amnesty international  walitoa taarifa kwamba Robert Mugabe na mpinzani wake Mkubwa nchini humo Morgan Tsvangirai hawana sifa za kugombea tena na hii ni kutokana na umri wao kuwa mkubwa sana Robert mugabe ana  umri wa miaka 93.
Grace Mugabe amesema haogopi kuchukua nafasi hiyo , akasema kama mume wake anataka kumpa kazi ampe bure yeye haogopi “ mimi siogogopi kama unataka kunipa nipe tu usiwe na wasiwasi na mimi” 
Taarifa zinasema makamu wa raisi wa nchi alitegemewa kupokea kijiti cha Uraisi kutoka kwa Rais Mugabe mwenye umri wa  miaka 93 lakini kwa sasa Makamu wa raisi hana mahusiano mazuri na Rais Mugabe na siku za karibuni Mugabe Alitangaza kumfukuza makamu  kwa kufanya njama za kutafuta watu wa kumsaidia katika uchaguzi mkuu ujao.
Chama kipo kwenye mpasuko  kwa sababu hawajui nani atakuwa Rais , GRACE MUGABE pia alisema hivi karibuni watabadilisha katiba ili iweze kuwaruhusu wanawake kuwa makamu wa rais.

Grace Mugabe anasema makamu wa Rais wa sasa alipanga njama mwaka 2014 za kuipindua serikali.

No comments:

Post a Comment

Note: only a member of this blog may post a comment.